Sheria haziwabani abiria
Kwa macho yangu nimeshuhudia abiria kadhaa waking'ang'ania kushushwa katikati ya barabara na konda alipokaa wakamtukuna. Ninachojiuliza ni kwamba, je, konda angewashusha wale abiria na jamaa wa Majembe wakamzukia wangelikubali kuwa kosa ni la abiria na sio konda.
Ushauri ili tutende haki kwa wot lazima tuwawajibishe pia na abiria.
**************************************************************************************************************************************
Kituo cha Mwenge
Ni vizuri kama kungelijengwa vituo vingine vya daladala ili kituo cha Mwenge kipumue. Sasa hivi kila daladala hulazimika kuingia hapo na kusababisha foleni nyingine ya kipumbavu.Ninashauri pawe na kituo kingine upande wa pili ili magari yote yanayotokea njia ya Ubungo yaishie na kugeuza hapo. Na kisha pajengwe kituo cha tatu mwanzo wa kuelekea njia ya Kawe/Lugalo kwa ajili ya mabasi yanayotokea Kawe, Tegeta, Bunju na Bagamoyo. Na kituo cha sasa kibaki kwa magari yatokeayo Ali Hassn Mwinyi na Sinza tu. Turahisishie daladala uwajibikaji kwa abiria wao na tuondoe viini vya magomvi yasiyokuwa na kichwa wala mguu !
**************************************************************************************************************************************
Maktaba St. na daladala.
WAKATI umefika wa kugeuza njia ya Maktaba kuwa njia moja na isiwe njia mbili. Magari yawe yanatoka tu kuja barabara ya Bibi Titi na sio kuingia. Badala yake magari yawe yanaingilia njia ya juu kwenye nyumba ya Sanaa na Move'n'pick [Royal Palm hotel ]na hapa yawe yanaingia tu na magari yasiruhusiwe tena kutoka. Kwa kufanya hivyo, maisha ya watumia mtaa wa Maktaba yatakuwa na nafuu kubwa.
**************************************************************************************************************************************
Urahisi wa kutnga sheria, kufuatilia je ?
Kuna wakati daladala zilitakiwa kuwa na kiboksi cha 'first-aid' haraka haraka wenye mabasi walieweka viboksi hivyo. Hata hivyo, kutokana na ufuatiliaji duni daladala nyingi hivi leo hazina maboksi ya 'first-aid' na badala yake kuna viboksi vilivyogeuka takataka na hatari kwa wapanda daladala kwa jinsi vinavyoning'inia ovyo.
**************************************************************************************************************************************
Daladala zinavyokwepa wanafunzi
Inasikitisha kuona baadhi ya daladala za Tabata zinavyoruka vituo pindi waonapo mlundikano wa wanafunzi. Huu si uungwana. Waafunzi nao ni abiria na wanaostahili kuhudumiwa kama wengine. La kuchekesha zaidi utakuta daladala haina watu lakini bado inawakataa wanafunzi. Pengine nauli ya sasa ni kubwa mno kiasi ambacho shilingi mia kwa daladala nyingine haina thamani?
**************************************************************************************************************************************
Lugha chafu
Uungwana katika dalaadala sio jambo linaloonekana tena sikuhizi. Kuna watu wengine ikiwemo pia madereva na makonda wa daladala inaelekea sala yao ya kwenda kulala, ya kuamka na ile sala wakiwa barabarani ni kuomba kuomba kugombana na watu wengine. Na katika hili hakuna anayenufaika ili kujenga roho mbaya itakayowatumbukiwa Watanzania wote baada ya miaka si mingi kutoka sasa.
**************************************************************************************************************************************
Simu na madereva wa daladala
Hivi majuzi nusra tuingie lori la tani 25 lililokuwa mbele yetu eti tu kwa sababu dereva wa daladala yetu alikuwa akiongea na tajiri kuhusu sijui ushuzi gani. Hivi hao ni matajiri njaa, hugonji dereva arudishe gari ndio mzungumze au mpange siku ya dereva kupumzika ili mpange vyema yanayowahusu ?
**************************************************************************************************************************************
No comments:
Post a Comment